Prince Harry na Meghan Kuanza Kujitegemea...Wanatakiwa Kulipa Bilion 70 Kama Kodi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kasri la Buckingham limetangaza rasmi kuwa Prince Harry na mkewe Meghan hawataruhusiwa tena kutumia vyeo vya kifalme walivyonavyo na hawatapokea tena fedha za Umma kwaajili ya shughuli za kifalme.

Mbali na hayo wawili hao pia hawatahusika tena na shughuli za kumwakilisha Malkia.

Aidha taarifa hiyo pia imeongeza kuwa watawala hao wa Sussex watatakiwa pia kulipa paundi milioni 2.4 sawa na zaidi ya shilingi bilioni 70 kama kodi kwaajili ya marekebisho ya makazi yao ya Frogmore Cottage ambayo yatakuwa nchini Uingereza.

Makubaliano hayo mapya yanatarajiwa kuanza rasmi mwezi Machi mwaka huu, kwa mujibu wa taarifa ya kasri.

Taarifa hiyo imekuja kufuatia mazungumzo yaliyofanyika mwanzani mwa juma hili kati ya Malkia na wawili hao kuhusu hatma ya maisha yao ya baadaye baada ya kutangaza kuwa wanataka kujitoa katika majukumu ya kifalme na kufanya shughuli zao kwa kujigawa kati ya Uingereza na Canada.



Katika sehemu ya taarifa hiyo Malkia amenukuliwa akisema ” kwa miezi kadhaa ya majadiliano na mazungumzo mengi ya hivi karibuni” nimeridhia” kwa pamoja kupatikana kwa suluhisho lenye kujenga na kusaidia namna ya kumwezesha mjukuu wangu na familia yake”.

“Harry, Meghan na Archie watakuwa wakati wote ni wajumbe wanaopendwa katika familia yangu ya kifalme,” iliendelea kueleza taarifa hiyo.

Amewashukuru kwa “kazi walizojitoa”, na kuongeza kuwa alikuwa “akijivunia namna Meghan alivyojitahidi kwa haraka kuwa mmoja wa wanafamilia.”

Lakini kwa upande wa wachambuzi wa mambo akiwemo Katie Nicholl, mwandishi wa kujitegemea wa jarida la Vanity Fair anayeandika masuala ya Kifalme amesema, kujitoa kwa Harry na Meghan katika shughuli za kifalme ni pigo kwa taasisi hiyo maarufu ulimwenguni.

“Watawala wa Sussexes wameshinda kwasababu wamepata walichotaka, ambacho ni Uhuru kutoka Faimilia ya Kifalme. Harry na Meghan wameweza kuleta maajabu na upekee kwa familia ya kifalme,” alisema Nicholi.

Amesema makubaliano hayo pia yanaweza kufungua njia kwa vijana wa kizazi cha sasa wa kutoka familia za kifalme katika miaka ijayo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad