AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mamlaka ya mapato TRA, Mkoa wa Ruvuma imemtoza faini ya shilingi milioni 9 mfanyabiashara anayesambaza pembejeo kwa wakulima kwa kosa la kuuza mbolea bila kutumia mashine ya kutolea risiti ya EFD kama sheria inavyotaka.
Aidha kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Simon Maigwa amesema jeshi hilo linamshikilia mfanyabiashara huyo kwa kosa la kuuza mbolea kinyume na bei elekezi ambapo urea ilipaswa kuuza kwa shilingi 54,500 lakini yeye anauza kwa shilingi 60,000.
Januari 23 mwaka huu, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo alifanya ziara kwenye maghala ya kuuzia mbolea kwa lengo la kujua kama wanafuata bei elekezi ya serikali.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK