Corona ni Ushahidi Kuwa Watumishi wa Afya Wanatakiwa Kulipwa Vizuri Kuliko Wengine

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mdau wa JamiiForums.com anasema hali ya #corona kwa nchi za Ulaya kwa sasa na hatari inayowakabili Watumishi wa sekta ya afya duniani ni ushahidi tosha kuwa kada hii ni kada muhimu na nyeti sana kuliko kada zingine zote

Anasema ni kweli karibu kila kada/kazi ina hatari zake, lakini kada ya afya ina hatari kubwa zaidi hasa yanapotokea majanga ya maradhi ya mlipuko kama ilivyo #Covid_19 kwa sasa

Sasa hivi watu tunaogopa hata kusogeleana huku tukiwa hatuna hata uhakika kuwa jirani zetu wana virusi lakini Madaktari na Manesi na Wafanyakazi wengine katika kada hii wao wanalazimika kuwahudumia wagonjwa licha ya hatari ya kupata maambukizi

Mbali na #corona, hata wanapohudumia wagonjwa wa magonjwa mengine, kama vile kuwafanyia upasuaj wagonjwa au kina mama wajawazito wenye magonjwa bado wanakuwa kwenye hatari kubwa tu ya wao kuambukizwa magonjwa hayo

Je, una maoni gani juu ya hoja ya Mdau?
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad