Habari Njema Kwa Watanzania..PATO la Taifa Lapanda kwa Asilimia 7

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Habari Njema Kwa Watanzania..PATO la Taifa Lapanda kwa Asilimia 7

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema pato la taifa limekuwa kwa asilimia 7 kwa mwaka 2019 sawa na ilivyokuwa kwa mwaka 2018.

Dkt. Mpango ameyasema hayo Bungeni mjini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kueleza sekta ambazo zinaongoza kwa ukuaji nchini.
Amezitaja sekta zilizoongoza katika ukuaji ni pamoja na uchimbaji wa madini na mawe kwa asilimia 17.7, ujenzi kwa asilimia 14.1, sanaa na burudani asilimia 11.2, usafirishaji na uhifadhi wa mizigo asilimia 8.7.
Katika hatua nyingine Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai aliikataa hotuba ya bajeti ya fedha na mipango ya kambi ya upinzani kutokana na Waziri Kivuli Mh. Halima Mdee kutokuwepo bungeni wakati baadhi ya wabunge waliokuwa wamejiweka karantini wamerejea bungeni.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad