Rais Magufuli Asema Ameuona Mkono wa Mungu Katika Kipindi hiki Kigumu Cha Corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais John Magufuli amesema anamshukuru Mungu kwa kujibu maombi katika pindi hiki kigumu cha ugonjwa wa Corona kwani ameuona mkono wake.

“Ameniagiza tena kwenu maneno aliyoyasema kutoka katika kitabu cha pili kutoka kitabu ya mambo ya nyakati 7:13. Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yakasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa,” alisema Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Paramagamba Kabudi kwa niaba ya Rais Magufuli.

Amesama Rais amemuagiza awajulishe waumini na watanzania wote kwamba anashukuru kwa jinsi walivyoitikia wito wa awali wa kutenga siku tatu za kuomba na sasa ni mahali pa kutoa shukrani kwa Mungu.

“Rais amesema ameuona mkono wa Mungu, Rais anasema ameuona miujiza ya Mungu, Rais anasema ameuona upendo wa Mungu na ameyaona maajabu yake kwa watu wake,”.

Aliongezea kusema kuwa “Rais mesema inawezekana yeye asijue kusali lakini anaamini kwa sala za Watanzania wote waliopiga magoti Mungu amewasikiliza na yeye kwetu kwa unyenyekevu mkubwa anasema asante sana Mungu wangu nauhimidiwe na ushukuriwe na uonekane kati ya mataifa yote,”.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Jemedari wetu Mwenye Maono na Msimamo
    usio tetereka na wengi wanaanza kukuelewa, hivi leo Hapa Cyril Ramaphosa amesha tangaza kuanzia Juni mosii atalegeza lokidawni to level 3.
    ambayo itafungua mambo mengi ikiwemo
    Uimarishaji waUchumi.

    JPJM Alikwisha yaona hayo from DAY ONE

    Eid Mubarak..!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mdau, Magu ni Gumzo la Dunia.
      Habari nyingine kabisa. Moto wa
      kuotea mbali.

      Aima'nyile Milimo Viswano Duu.
      Uwalamsaje woose kukaya duu.

      Long live Mdodo wetu Magu.
      Mlungu Akuta'zee Gweee.

      Uwalamsaje KwiDodoma.

      Allah akulinde Magu wetu na Mahasidi wanapo Husudu.

      Eid Mubarak.

      Delete

Top Post Ad