AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Raisi mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amempongeza sana Raisi John Magufuli kwa kufanya mambo mengi, mapya na mazuri.
Akisalimia wananchi wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi za ikulu Dodoma, mzee Mwinyi amesema Rais Magufuli anatumia fikra za ujana kufanya mambo makubwa nchini.
Baadhi ya mambo mapya na makubwa aliyofanya Raisi Magufuli ni kuhamishia serikali na wizara zote Dodoma na kujenga ikulu mpya Dodoma.
Raisi Magufuli pia anajenga mradi mkubwa wa umeme unaoitwa Mwalimu Nyerere Hydro power Project wenye zaidi ya megawati 2000 katika bonde la Rufiji.
Rais Magufuli pia amewasha umeme katika zaidi ya vijiji elfu nane tangu aingie madarakani.
Kama hiyo haitoshi Rais Magufuli yupo anajenga treni ya mwendo kasi kutoka Dar es salaam mpaka Mwanza ambapo kipande cha kwanza kutoka Dar es salaam hadi Morogoro kitazinduliwa hivi karibuni.
Yapo mengi amefanya Raisi katika kipindi cha miaka mitano angani, ardhini na majini ila nafasi haitoshi kuandika vyote hapa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Alhajj Ali Hassan, Mcha mungu na msema
ReplyDeletekweli Alie na Busara na Hekima.
Babba Ruksa, Swadakta kwa Magu wetu
yote uliyo sema.Ana Maono na Uthubutu.
Mwenyezi mungu akupe Afya na Atulindie
kipenzi chetu Performance Driven Magu.