AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
NCHI za Tanzania na Kenya zimeafikiana kuwa madereva watatakiwa kupimwa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona katika nchi zao na kupewa cheti maalum kitakachowatambulisha kutokuwa na maambukizi ambacho kitakuwa halali kwa siku 14 pekee.
Baada ya siku hizo kukamilika, madereva hao watalazimika kupimwa tena wakiwa nchini Kenya au Tanzania na endapo watagundulika, watarudishwa katika nchi zao.
Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwele leo, Ijumaa, mpakani Namanga baada kumalizika kikao kilichomjumuisha Waziri wa Uchukuzi wa Kenya, James Macharia.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK