Rais Ampongeza Bilionea Mpya wa Madini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Rais John Magufuli amempongeza mchimbaji mdogo wa madini, Saniniu Kurian Lazer  ambaye leo ameiuzia serikali madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilogramu 15 na thamani ya Sh bilioni 7.74.

Ametoa pongezi hiyo alipompigia simu Waziri wa Madini, Dotto Biteko wakati serikali ikikabidhiwa madini ya Tazanie yenye thamani ya Sh bilioni 7.8 iliyoyanunua kwa mchimbaji Laizer.

“Hongera Laizer, najua unakwenda kutafuta mwanamke mwingine ukatafute mke wa Kisukuma,” amesema Magufuli wakati akizungumza na bilionea huyo.

Katika madini hayo, Jiwe moja lenye uzito wa kilo 9.2 lina thamani ya Sh bilioni 4.5 na lingine lina uzito wa kilo 5.8 lenye thamani ya Sh bilioni 3.3.

 Aidha Waziri Biteko amesema Laizer ameyatoa mawe hayo umbali wa mita 1,800 kutoka usawa wa ardhi ambapo Rais Magufuli aliagiza serikali inunue madini hayo.

Serikali tayari imemkabidhi Laizer mfano wa hundi ya Sh bilioni 7.744 na kwamba fedha hizo zitawekwa kwenye akaunti yake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad