Serikali Yataifisha Dhahabu ya zaidi ya Tsh. Billion 2.9

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Serikali imetaifisha dhahabu ya Kilogram 27.488 yenye thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni 2.9 iliyoingizwa kinyemela kutoka Kenya
-
Dhahabu hiyo mali ya Mfanyabiashara Bhawesh Chandulal Gandecha, ilikamatwa na Afisa Forodha katika mpaka wa Tanzania na Kenya huko Sirari, Mei 15, 2020
-
Meneja wa TRA Mkoa wa Mara, Wallace Mkande, amesema Mfanyabiashara huyo alikamatwa akitaka kuingiza dhahabu hiyo kutoka Kenya kinyemela bila kuwa na nyaraka za kuonesha amelipia ushuru
-
Mfanyabiashara huyo alipoulizwa alisema ameshalipa ushuru ila hajapewa stakabadhi na kuwa nyaraka nyingine zipo Dodoma huku akipiga simu kwa baadhi ya watu kuwalalamika kwa kushelewesha kuzituma
-
Alifunguliwa kesi Uhujumu Uchumi katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime na kushtakiwa kwa makosa ya Kuendesha Mtandao wa Uhalifu, Kufanya biashara ya dhahabu bila nyaraka muhimu na kutakatisha fedha

#JamiiForums - #regrann
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad