Agizo la Rais Uwanja wa Mkapa laanza kutekelezwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo imeanza kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli kubadili jina la uwanja wa Taifa kumuenzi Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamini Wiliam Mkapa.

Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo imeanza kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli kubadili jina la uwanja wa Taifa kumuenzi Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamini Wiliam Mkapa.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Yusufu Singo, na kueleza kuwa mchakato umeshaanza na wameshaliondoa jina la zamani ili kuweka jina la Benjamini Mkapa, kwa maelekezo ya Waziri wa Michezo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

'' Baada ya maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt John Pombe Magufuli kutaka uwanja huu ubadilike ili tuweze kumuenzi Rais wa awamu ya Tatu, Hayati Benjamini Mkapa, tayari Waziri mwenye dhamana ya michezo na katibu Mkuu wa Wizara ya michezo, wameelekeza tuanze shughuli hiyo mara moja na tumeanza kuliondoa jina la zamani la 'National Stadium.'' Alisema Singo.

Singo ameongeza kuwa baada ya kuliondoa jina la zamani la uwanja huo, lakini kuna changamoto kidogo ya kuliweka jina jipya hivyo wanasubiri kukutana na wataalam wa Wizara, huku mafundi wakiwa tayari wanaendelea na ujenzi kwenye eneo husika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt John Pombe Magufuli alitoa maelekezo ya kubadili jina la uwanja wa Taifa, uitwe Uwanja wa Benjamini Mkapa, wakati akitoa salamu za rambirambi kwenye kuuaga mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamini Wiliam Mkapa, Jumanne hii kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad