Google Yatuhumiwa Kuingilia Faragha za Watumiaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Google na kampuni yake Mama iitwayo Alphabet Inc wameshtakiwa kwa kuingilia faragha za mamilioni ya watumiaji wake kinyume na utaratibu na kutakiwa kulipa fidia ya dola bilioni 5

Walalamikaji wanasema Google imekuwa ikikusanya taarifa za watumiaji wakiwa 'online', kujua wanatafuta nini, taarifa gani wanafuatilia na wanafanya nini kwenye 'App' zao hata wakiwa kwenye 'private mode'

Aidha, shtaka linaeleza kuwa hata pale wateja wanapofuata maelekezo na kuzima nyenzo zote za kufuatiliwa bado Google huendelea kufuatilia na kuingilia shughuli zote zinazofanywa na wateja wake katika wavuti mbalimbali

Ukusanyaji wa data hizo husaidia Google kujua maisha ya faragha ya kila mtu mwenye simu au kompyuta ikiwemo kujua marafiki zao ni akina nani?, wanapenda kula nini?, kununua nini?, na hata kujua vile vitu vya aibu mtu alitafuta 'online'

Hadi sasa bado Google hawajatoa maelezo yoyote kufuatia tuhuma hizo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad