Hatimaye Lulu Michael Afunguka Kinachokwamisha Ndoa yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Staa wa Filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amesema kuwa aharakishi kuingia kwenye ndoa kutokana bado kuna vitu anahitaji kufanya yeye kama msanii, hivyo atakapoingia kwenye ndoa hataweza kutekeleza hayo vizuri.

Lulu ameeleza hayo jana pale alipodakwa na wanahabari akitokea katika hafla ya uhamishaji wa COSOTA kutoka Wizara ya Viwanda kwenda Wizara ya Habari ili kuziweka pamoja mamlaka zinazosimamia wasanii.

“Sidhani kama kuna haja ya mimi kuharakisha kukimbilia kwenye ndoa, kwanza mashabiki zangu wanatakiwa watambue #Lulu ni 'brand', nina maisha yangu binafsi ya kuyajenga.” ameeleza.

“Wote tunajua ukishaingia kwenye ndoa ni jukumu lingine kubwa sana ambalo nikili harakisha itabidi nijikane mimi kama 'brand', itafika siku tu, #Lulu ataolewa, atakuwa na ndoa,” aliongeza Lulu.

Itakumbukwa, Lulu alishavishwa pete ya uchumba na Francis Ciza maarufu kama #Majizzo, mwishoni mwa Septemba 2018 na siku kadhaa baadaye alitolewa mahari na mchumba wake huyo na kinachosubiriwa hivi sasa ni harusi yao tu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad