Haya Hapa Madhara ya Kunywa Damu (Kisusio)

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kama ukinywa damu kasi kidogo sana (labda vijiko vichache vya chai), na iwapo damu hiyo haina vijidudu vya bakteria au virusi vya magonjwa, basi damu hiyo yaweza isiwe na madhara kiafya. Kama damu hiyo ni nyingi na pia huna hakika kuhusu usalama wake dhidi ya vijidudu, usinywe.

Jambo la ajabu ni kwamba, damu unapoinywa ni sumu. Kama damu ikiwa kwenye viungo vinavyohitaji damu — kama moyo, mishipa ya damu na vingine — inakuwa na umuhimu mkubwa kwa kiumbe hai. Lakini ikinywewa inakuwa ni hadithi tofauti kabisa. Inabidi ieleweke kwamba kila sumu inahitaji dozi fulani iweze kuonesha madhara yake, ni sawa na kwamba unaweza usidhurike utakapokunywa tone moja la sumu lakini unapoongeza kiasi, hatari inakuwa kubwa zaidi.

Kwa sababu damu ina kiwango kikubwa sana cha madini ya chuma — na kwa sababu mwili unapata tabu kutoa madini ya chuma yaliyozidi — mnyama yeyote anayekunywa damu mara kwa mara anakuwa kwenye hatari ya kuwa na kiasi kikubwa cha madini haya. Ingawa madini ya chuma ni muhimu sana kwa wanyama wote (na kwa kila kiumbe hai), yanapozidi huwa ni sumu inayoweza kusababisha magonjwa kama magonjwa kama homa ya ini (aina B na C), mapafu kujaa maji, kupungua kwa maji mwilini, shinikizo la chini la damu, matatizo ya mfumo wa fahamu, magonjwa mbalimbali ya zinaa pamoja na UKIMWI.

Tofauti na binadamu, miili ya wanyama ina uwezo wa kumeng’enya damu kwakuwa ina mfumo maalum wa kuwezesha kazi hii. Wanyama wanaokunywa damu wanahitaji kiasi kikubwa cha madini ya chuma yanayomsaidia kutengeneza sukari inayobeba hewa ya oksijeni kutoka kwenye mapafu kwenda kwenye tishu mbalimbali za mwili.

Kwa wanyama kama popo, damu wanayokunywa inakuwa nyingi kuliko inayohitajika mwilini, kwahiyo kuna mfumo maalum wa kuitoa. Wanapoinywa, damu inapita kwenye njia maalum inayonyonywa virutubisho. Tafiti zimeonesha kwamba mfumo huu una ukuta wa majimaji kwenye utumbo ambayo ina uwezo wa kuzuia madini ya chuma yasiingie kwa kiasi kikubwa kwenye mfumo wa damu.

Sisi binadamu si kama popo kwa sababu hatuna mfumo wa kusaidia kudhibiti kiwango cha madini ya chuma kinachoingia mwilini, kwahiyo damu itatuua.

Kama ukipata jeraha dogo la kuchanika midomo na kwa bahati mbaya ukanywa kiasi cha vijiko vichache vya damu yako au iwe unapenda kunywa damu za wanyama kama ng’ombe, mbuzi au kondoo wanapochinjwa, ni bora ukajua madhara ya kiafya yanayotokana na kunywa damu hiyo hata kama ni kiasi kidogo. Yawezekana ni muhimu sana kutufanya tuwe hai ikisukumwa na moyo au kupita kwenye mishipa ya damu lakini itakuchukua uhai huo kama ambavyo sumu yoyote ile itavyofanya utakapokuwa na tabia ya kuinywa mara kwa mara.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad