Ibada ya Hijja inaanza Leo kwa idadi ndogo ya Waumini wa Kiislamu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Makka, Ibada ya kila mwaka ya Hijja inaanza leo katika mji mtukufu wa Makka nchini Saudi Arabia chini ya kiwingu cha janga la virusi vya corona lililosababisha kupunguzwa kwa idadi ya watu watakaoshiriki ibada hiyo.

Waislamu wasiopindukia 10,000 ambao tayari wanaishi nchini Saudi Arabia ndiyo watashiriki Hijja inayofanyika kwa siku tano, idadi ambayo ni sehemu ndogo ya mahujaji milioni 2.5 waliohudhuria mwaka uliopita.

Vyombo vya Habari vya Taifa vimeonesha wafanyakazi wa afya wakipuliza dawa ya kupambana na virusi kwenye masanduku ya mahujaji huku wengine wakipatiwa mikanda maalum ya kufuatilia mahali waliko.Kwa lengo pia la kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona, mamlaka inayosimamia ibada ya Hijja pia imepiga marufuku kwa mahujaji kuligusa ´´Ka´bah´´ jengo dogo la mraba lililo katikati ya msikiti mkuu wa mjini Makka.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad