Jacqueline Mengi afunguka kuhusu kuolewa tena

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mwanadada Jacqueline Ntuyabaliwe ambaye ni mjane wa Reginald Mengi, Jumatatu hii amejibu maswali ya mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo aliwapa fursa ya kuuliza chochote na wengi wakatiriria. 

Katika sehemu hiyo ya maswali na majibu, vitu ambavyo huenda vikawashangaza wengi ni namna alivyoweka wazi umri wake kitu ambacho wadada wengi hupenda kutosema miaka yao. 

Kwenye moja ya swali aliloulizwa na shabiki yake nikuhusiana na umri wake kwa sasa, Jacqueline bila kificho alimjibu SHABIKI huyo kuwa, “Nina miaka 41 ila najihisi kama nina miaka 21.” aliandika. 

Pia mrembo huyo ambaye ni mama wa watoto wawili mapacha hakusita kuongelea masuala ya ndoa ambapo shabiki mmoja alimuuliza, “Utaolewa tena?” naye akajibu, “Sijui, ngoja tuone Mungu amenipangia nini.” 

Mbali na hayo, shabiki mmoja alimuuliza kama anaweza kuingia kwenye Siasa siku moja, Jack hakusita kujibu swali hilo akiweka wazi kuwa, havutiwi kabisa na masuala ya Siasa, “Hapana, sina interest nayo kabisa” aliandika.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad