Joe Biden "Donald Trump Ndiye Mbaguzi wa Kwanza wa Rangi Kuwa Rais wa Marekani"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mgombea wa urais Marekani kwa chama cha Democratic Joe Biden amesema Rais Trump ndiye mbaguzi wa kwanza wa rangi kuwa rais wa Marekani. Kauli hiyo imekanushwa vikali na timu ya kampeni ya Trump.

Biden ambaye alikuwa makamu wa rais katika uongozi wa Rais Barack Obama, Mmarekani mweusi wa kwanza kuwa rais alikuwa anajibu swali la muhudumu mmoja wa afya aliyeuliza kuhusiana na Rais Trump kuviita virusi vya corona, virusi vya China.

Biden amesema katika historia hakuna rais wa Marekani ambaye ashafanya kitu kama hicho. Vita hivi vya maneno kati ya Biden na Trump vinazidi ukizingatia kuwa suala la rangi ni nyeti sana na limekuwa likizungumziwa sana.

Biden na Trump wote ni watu weupe na mmoja kati yao anatarajia kuwa rais wa Marekani baada ya uchaguzi wa Novemba 3.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad