Kesi ya Mkurugenzi wa Jamii Forums Kutajwa Tena Leo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kesi namba 458 ya mwaka 2016 (Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi wa Jamii Forums na Mwanahisa wa Jamii Media) inatajwa tena leo, Julai 30, 2020 asubuhi mbele ya Hakimu Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar

Mara ya mwisho iliposikilizwa Juni 25, 2020 Jamhuri iliiomba Mahakama iruhusu kukamatwa kwa Shahidi Tully E. Mwambapa ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano kwa Umma (CRDB) kufuatia kesi hiyo kuahirishwa kwa takriban mara 9

Katika shtaka la kwanza, Mkurugenzi wa Jamii Forums anatuhumiwa kuendesha mtandao (JamiiForums.com) ambao haujasajiliwa Tanzania na vile vile hautumii Kikoa cha do-TZ

Katika shtaka la pili la Shauri hili, Polisi ilimtaka Mkurugenzi wa Jamii Forums kutoa taarifa kuhusu Wanachama wawili wa Mtandao wa JamiiForums.com waliodaiwa kuandika kuhusu madai ya uhalifu uliokuwa ukiendelea katika Benki ya CRDB

Taarifa zilizotakiwa ni IP-Address, barua pepe, Majina Halisi ya Wanachama hao. Pia ilitakiwa zitolewe post zote zinazohusu Uhalifu unaofanyika CRDB kitu ambacho Polisi wanadai Mkurugenzi huyo aligoma kuwapa
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad