Kizimbani Kwa Kuwaingizia VIDOLE Sehemu za Siri Watoto Wadogo 7

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Irene James (36) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora akituhumiwa kuwafanyia unyanyasaji wa kingono watoto 7 wa kike wenye umri kati ya miaka 4 hadi 7 kwa kuwaingizia vidole sehemu za siri

Mtuhumiwa huyo aliwatendea makosa hayo watoto wa majirani zake kwa nyakati tofauti majira ya mchana kati ya Januari hadi Julai mwaka huu katika Kata ya Kanyenye

Makosa hayo ni kinyume cha Kifungu cha 138 C (1) (a) na Kifungu kidogo cha 2(b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019

Kutokana na Sheria hiyo Mtuhumiwa akipatikana na hatia atawajibika kwa kifungo kisichopungua miaka 25 na kisichozidi miaka 30 na pia atalipa fidia kwa kiwango kitakachoamriwa na Mahakama

Aidha, Mahakama hiyo imemnyima dhamana mshtakiwa kwa madai ya usalama wake na kwamba amepelekwa mahabusu mpaka pale kesi hiyo itakapotajwa tena Agosti 13
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad