Mama Sepetu Asakwa kwa Kuharibu Nyumba ya Serikali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




MJANE wa aliyekuwa Makamu Jaji Mkuu wa Zanzibar, Jaji Mkusa Isaac Sepetu, Mama Salma Mkusa Sepetu, anasakwa na vyombo vya dola kwa tuhuma ya kuharibu vibaya nyumba ya Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC) aliyokuwa akiishi na familia yake baada ya shirika hilo kumtaka ahame.

 

Imeelezwa kuwa baada ya mumewe kufariki alipewa notisi ya kuhama, lakini aliomba aachwe kwanza katika nyumba hiyo ambayo alidai kuwa walitumia gharama kubwa kuiremba na kuitia mapambo ya kila aina na kwamba hakuwa na deni.  Hata hivyo, ombi lake lilitupiliwa mbali.

 

Imeelezwa kwamba, mama huyo alitoa malalamiko akidai kwamba ZHC ilimtaka kuhama na kukabidhi funguo za nyumba waliyokuwa wakiishi na marehemu mume wake maeneo ya Michenzani Block namba 9/116.

 


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad