Unaambiwa Baba wa Beyonce Alishtukia Mchezo Mchafu wa R Kelly Mapemaa na Kuamua Kuminda Mtoto Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


BABA wa Beyonce, Mathew Knowles, ameweka wazi kuwa alikuwa makini kumlinda mwanawe huyo na Kelly Rowland, wakati wanafanya kazi na staa wa muziki wa RnB, R. Kelly.

Knowles ambaye alikuwa meneja kwenye tasnia ya muziki, aliwahi kufanya kazi na R. Kelly mwaka 1998, huku Beyonce na Kelly Rowland wakiwa na umri wa miaka 17.

“Nilikuwa makini sana wakati nafanya kazi na R. Kelly, ilikuwa mwaka 1998, wakati warembo hao wakiwa na umri wa miaka 17, sikutaka kuwaacha peke yao, mara zote nilikuwa namwambia mke wangu Tina aungane nao kokote aendako hata kama bafuni kuliko kuwaacha wakiwa na R. Kelly.

“Kwa kufanya hivyo, warembo hao walikuwa sehemu salama, muda mwingi nilikuwa nao studio huku nikiwa na R. Kelly, lakini hakuweza kufanya lolote,” alisema Knowles.

R. Kelly kwa sasa yupo katika wakati mgumu kutokana na kashfa zake za unyanyasaji wa kingono.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad