Unachopaswa Kufanya Katika Hatua Za Awali Za Uhusiano Na Msichana Unaempenda..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kwa kawaida Mwanaume unapohitaji kuanza uhusiano na msichana unaempenda sana, kiu na njaa ya kuwa naye huwa iko katika kiwango kisichopimika.

Hasa unapokuwa unaanza kuwasiliana nae na ukafanikiwa kumsogeza karibu na kumuonesha kwa vitendo kuwa unampenda na kwa bahati nzuri, akaanza kukuwashia ‘Taa ya Kijani’.

Hata hivyo, mwanzo huu unaweza kuwa mbaya kwako endapo hautazingatia kanuni moja muhimu sana kati ya kanuni nyingi za kuendeleza na kudumisha mapenzi yaliyochipua yanayohitaji mbolea na maji safi kutoka kwako ili yachanue.

Ingawa ukweli ni kwamba muonekano wake na mvuto alionao mwanamke unaempenda unaweza kuwa ndio chanzo kikubwa kilichokusukuma kumfuata na kuanzisha maongezi kwa mara ya kwanza, ni muhimu sana kutomuonesha dalili zozote kuwa ‘ngono’ ndio hitaji lako la kwanza au kitu ulichokipa kipaumbele.

Kabla hujamwambia kitu chochote, kumbuka yule ni mtu mzima, mrembo aliyewavutia wengi kabla yako. Jiulize maswali kadhaa, je, kwa makadirio ya haraka haraka unadhani kuna neno jipya utakalomwambia ili akuamini wewe tofauti na wanaume wengine waliowahi kuongoa naye?

Hapo ndipo utagundua kuwa maneno yako yana nafasi ndogo sana kwake hivyo unapaswa kuyachagua kwa umakini mkubwa ili yapenye masikio yake na kuyahifadhi kwa muda ili ayatafakari kabla hayauruhusu moyo wake kuyatafrisi.

Wataalam wa masuala ya mahusiano wanashauri kuwa lugha ya mwili (body language) inaongea kwa sauti zaidi ya sauti yako. Hivyo, unapaswa kujiweka vizuri tangu unapomuangalia, unapomsalimia, mwili wako unapaswa kuongea kitu.

Hii inakuwa rahisi sana kama moyo wako umempenda kweli, mwili huongea wenyewe bila kuulazimisha.

Wanawake wengi wanajua kuzisoma lugha za mwili hata kabla ya lugha ya sauti. Hata hivyo, mioyo yao huwa migumu kuamini kile wanachokiona au kukisikia hususan kama wameshawahi kuumizwa mara kadhaa (kitu ambacho kipo kwa wanawake wengi hasa warembo).

Hata hivyo, baadhi hujikuta wanakupa nafasi ya kukusikiliza baada ya kugundua kuwa wewe unaonesha kupenda kweli tangu machoni. Imani ambayo huwepo kwa muda tu huku wasiwasi wa kuwa huenda unadanganya unakuwa juu zaidi.

Maneno na vitendo vyako vitakusaidia sana katika kuuteka moyo wa msichana unaetaka kuanzisha nae uhusiano ‘serious’ hivyo yachague kwa umakini. Tumia muda fulani mdogo kumsoma anachopenda, story anazopenda kuongelea na sehemu anazopenda kutembelea. Fahamu pia aina ya filamu anazopendelea na mengine ili uweze kuwa aina ya mwanaume unayeweza kucheza kila ngoma atakayokupigia katika mtiririko wa maisha.

Utafiti huo utakurahisishia maisha, na endapo utakaa naye vizuri na uhusiano wenu unaweza kuanza hata bila kumwambia maneno mengi. Yaani vitendo vikaongea hata bila kutumia maneno yanayotafsirika kama ‘kutongoza’. Kitakachofuata ni kumwambia maneno machache ili asikie alichokuwa anataka kusikia kutoka kwako. Funguka, na mwambie kiunaga ubaka.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad