AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
KIJANA aliyemtukana Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dkt John Magufuli katika mtandao wa Facebook amehukumiwa kulipa faini ya shillingi millioni 5 au kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kukutwa na hatia hio.
Kijana huyo anaetambulika kwa jina la Fadhili Silwimba, ni mkazi wa kijiji cha Nzoka Wilayani Momba Mkoani Songwe.
Hakimu Mkazi Mfawidhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe, Kassim Mkwawa, amesema mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 23(I) na (II) cha mwenendo wa makosa ya kimtandao namba 4 ya mwaka 2015.
Awali mwendesha mashtaka wa Serikali, Flavian Leonard Chacha, alisema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo, mnamo Septemba 7, 2019, kwa kutuma ujumbe wa kumtusi Rais kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK