Breaking: Aliyekuwa kocha wa yanga afungiwa miaka miwili na apiwa faini ya milioni 8

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kamati ya maadili ya shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) leo imetangaza kumuadhibu aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga SC raia wa Ubelgiji Luc Eymael kwa kumfungia miaka miwili kufanya kazi za soka nchini.

Pamoja na adhabu hiyo aliyopewa Luc Eymael amepigwa faini ya Tsh milioni 8 kutokana na makosa yake aliyoyafanya ya kutoa kauli zilizotafsiriwa kuwa za kibaguzi na kufanya Yanga SC kumfuta kzi mara moja.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Luc Eymael alitoa kauli za kibaguzi siku ya mchezo wa mwisho wa Yanga wa Ligi Kuu dhidi ya Lipuli FC mkoani Iringa.

Hata hivyo Luc Eymael amekuwa ni kocha anayeingia katika migogoro ya mara kwa mara na waajili wake kwani Kenya katika klabu ya AFC Leopards aliondolewa kwa aibu na kufungiwa mlango.

Afrika Kusini pia kupitia chama chao cha soka SAFA wameiunga mkono Yanga SC na TFF kwa kumuadhibu Luc Eymael kutofanya kazi nchini kwao kwa kosa alilofanya Tanzania la ubaguzi wa rangi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad