Dude apata ajali, akimbizwa Hospitalini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Msanii wa filamu Bongo Kulwa Kikumba maarufu kama Dude amekimbizwa Hospitali ya Magomeni Jijini Dar es Salaam baada ya kupata ajali ya bodaboda kwa kugongwa na gari la kubebea wagonjwa Ambulance.


Katibu wa wasanii wa filamu Jafari Makatu ameeleza kuwa, Dude alikuwa anawahi gari la wasanii ambao wanasafari ya kwenda Dodoma, alivyofika Magomeni Usalama akapata ajali iliyomsababishia majeraha kichwani.


"Kwa sasa tupo Hospitali Magomeni, alikuwa kwenye bodaboda akagongwa na Ambulance yeye na dereva wake wote wapo hospitali, amepata majeraha kichwani kwa hiyo ametoka kupiga Xray tunasikilizia majibu kama itashindikana tutamuhamishia Hospitali ya Rufaa wasanii wenzake wote wapo hapa hospitali, mwanzo alikuwa hawezi hata kuongea ila sasa hivi anaendelea vizuri kidogo" ameeleza Katibu wa wasanii Jafari Makatu 



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad