Fahamu jiwe la ekari 7 lenye ramani ya bara la Afrika linalotumika katika ibada za kimila Tanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Huwenda umepata kusikia maajabu mengi duniani hebu fahamu na hili, huko Mkoani Njombe Kusini Magharibi mwa nchi ya Tanzania kuna jiwe kubwa kwa jina la Lwiwala lenye ramani ya bara la Afrika.

Jiwe hilo la ukubwa ekari 7.8 limejizoelea umaarufu mkubwa kutokana na kuwepo kwa ramani ya bara la Afrika ambayo haijachorwa na mtu.

Katika mahojiano yake na Shirika la habari la BBC Mhifadhi Msitu wa Lwiwala, Yuda Masamaki amesema kuwa wakazi wa kijiji hicho hulitumia jiwe hilo katika ibada za kimila.

”Limepewa jina Lwiwala kwa sababu humeremeta nyakati za usiku, baadhi ya wakazi hutumia jiwe hilo kama madhabahu ya ibada zao za kimila,” amesema Yuda Masamaki ambaye ni Mhifadhi Msitu wa Lwiwala.

Masamaki ameongeza ”Humu kuna ramani ya Afrika ambayo haijachongwa na wanakijiji, isipokuwa ilitambuliwa na wataalamu.”


Jiwe hilo lenye ramani ya Afrika maarufu kama Lwiwala hutembelewa na watalii mbalimbali huku wageni wakitozwa dola 25 za Kimarekani huku wazawa dola mbili pekee.

Bongo 5
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad