google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html JPM Amsamehe Mkurugenzi Ikwiriri Aliyedanganya Gari ni Bovu | UDAKU SPECIAL

JPM Amsamehe Mkurugenzi Ikwiriri Aliyedanganya Gari ni Bovu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Pwani : 

Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, amemsamehe Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rufiji, Brighton Eliud Kilimba, aliyetoa taarifa za uongo kuwa gari la Kituo cha Afya Ikwiriri haliwezi kutembea wakati akizungumza na wananchi alipopita Ikwiriri Rufiji mkoani Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kamanda wa mkoa wa kipolisi Rufiji, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Onesmo Lyanga amesema uchunguzi ulifanyika kwa gari lenye namba za usajili STL 940 aina ya T/land Cruiser la Kituo cha Afya Ikwiriri, limegundulika lina uwezo wa kutembea na siyo kama taarifa aliyotoa kaimu mkurugenzi kuwa ni bovu.

“Tulimkamata tarehe 01.08.2020 kwa kosa la kutoa taarifa ya uongo na utaratibu wa kumfikisha mahakamani kwa kosa hilo ulikuwa unakamilishwa, leo amepata bahati, rais ameamua kumsamehe na kwasasa yuko huru,” Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Onesmo Lyanga
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad