Kesi ya aliyefanya mauaji katika msikiti wa New Zealand yaanza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kesi ya gaidi Brenton Tarrant, aliyewauwa watu 51 na kujeruhi watu 49 katika shambulizi  la silaha kwenye misikiti 2 huko Christchurch, New Zealand, imeanza.


Siku ya kwanza ya kusikilizwa kwa kesi hiyo imeanza katika Mahakama Kuu ya Christchurch, ambapo adhabu ya gaidi Tarrant itaamuliwa.


Kusikilizwa kwa kesi hiyo kunatarajiwa kudumu kwa siku 4, chini ya hatua kali za usalama.


Barabara ya kuelekea mahakamani imeonekana imejaa na ndugu na jamaa za wale waliopoteza maisha na kujeruhiwa huku polisi wakiwa wameweka ulinzi.


Gaidi, atakayehukumiwa na jaji wa Mahakama Kuu ya Christchurch, Cameron Mander, atahudhuria kusikilizwa kwake kupitia mfumo wa video na sauti kutoka Gereza la Auckland ambapo ameshikiliwa.


Gaidi huyo Tarrant, ambaye ombi lake la kujitetea lilikubaliwa na Mahakama Kuu ya Christchurch mnamo Julai 13, alikuwa amekubali mashtaka yote dhidi yake, pamoja na mauaji 51, majaribio 40 ya mauaji, na shambulizi moja la kigaidi.


Gaidi huyo anatarajiwa kuhukumiwa kifungo cha maisha baada ya siku 4 za mashtaka.


Tarrant alishambulia msikiti wa Nur na Linwood kwa silaha huko Christchurch wakati wa sala ya Ijumaa mnamo Machi 15, 2019, ambapo watu 51, mmoja wao akiwa ni raia wa Kituruki, walipoteza maisha na watu 49 walijeruhiwa, wakiwemo Waturuki wawili.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad