Kisa cha Kijana wa Shule Aliyenaswa Akimsugua Mke wa Mchungaji Katika Shamba la Mahindi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kijana huyo na mke wa mchungaji walinaswa wakipokezana asali katika shamba la mahindi

Kisa hicho kilifanyika muda mfupi baada ya ibada ya Jumapili

Wawili hao walikuwa njiani kuelekea nyumbani waliopoingia katika shamba la mahindi

Waumini wa kanisa moja katika kaunti ya Bomet wamesalia kwa aibu na mshangao baada ya muumini mwenye umri wa miaka 20 kufumaniwa akimla mke wa mchungaji katika shamba la mahindi.

Katika kisa hicho kilichofanyika Jumapili, Agosti 9, Bomet KENYA, wawili hao wanadaiwa kutoroka kanisani pamoja kurudi nyumbani baada ya ibada kabla kupatikana wakipokezana mabusu na manono shambani humo.

Inadaiwa kuwa mchungaji hakuweza kuandamana na mkewe nyumbani baada ya kualikwa kufanya mambo maalum kwa muumini, mkewe akiomba nafasi kurudi nyumbani upesi kushughilikia jambo la dharura.



Vincent Langat, mmiliki wa shamba kulikofanyika kisa hicho alieleza kuwa wanawe wawili walimuita nyumbani wakimjuza kuwa wezi walivamia shamba lao kuiba maharage.

‘’ Wanangu wawili waliniambia kuwa waliona watu wawili wakiingia shambani  lakini sikuwaamini, hapa hakuna mtu anayeiba hivyo nikachukua muda kidogo kabla kufika shambani.  Nilipokaribia, nisikia wawili hao wakivamiana bila huruma,’’ alisema

Nilifika karibu ndipo nikagundua alikuwa mke wa mchungaji, nililazimika kuwaita wengine kuja kushuhudia kisa hicho cha aibu.

Kijana huyo alitoka mbio baada ya kunaswa, akihofia aibu na mapigo.

‘’ Nimekuwa nikishuku  hili lakini nimesalia kimya . Ni vizuri leo imebainika,’’ Amos, mshiriki wa kanisa hilo alisema.

Mchungaji huyo alikataa kuzungumza kuhusu kisa hicho, chifu wa eneo hilo Samwel Rotich akiwatahadharisha wanaume dhidi ya tabia kama hizo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad