Kizza Besigye Akataa Kuchuana na Museveni Katika Urais 2021

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Chama cha The Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda kimejipata katika njia panda baada ya muasisi wa chama hicho na mgombea mara nne wa urais , Kizza Besigye, kukataa ombi la kupeperusha tena bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa ujao wa 2021.

Dkt Besigye, ambaye alipambana na Rais Museveni katika chaguzi nne za urais zilizopita tangu mwaka 2001, kila mara alimshutumu Rais huyo kuiba kura.



Alikwenda mara mbili katika Mahakama ya juu mwaka 2001 na 2006 na katika kesi zote hizo kwa kauli moja Majaji walithibitisha kuwa kulikua na wizi wa kura lakini kwa mgawanyiko wa kura mwaka 5:2 na 4:3 mwaka 2006 , huku wengi wa majaji wakiamua kuwa wizi wa kura haukutosha kubatilisha matokeo ya mwisho ya kura.

Uamuzi wa Dkt. Besigye wa kutogombea urais mwaka 2021 umekiacha Chama cha FDC kikimtafuta atakayekiwakilisha katika uchaguzi huo, ayari chama hicho kimeaihirisha mara mbili uteuzi wa wagombea wake wa uraiskwa matumaini kuwa Dkt. Besigye angebadili msimamo wake na kuchukua fomu za uteuzi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad