Kwanini si vizuri kulala kitanda kimoja na mtoto

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mama mmoja ametoa onyo kwa akina mama ambao huwa wanalala na watoto wao mara baada ya mtoto wake wa kiume mwenye wiki sita kufa na ripoti ya uchunguzi wa kifo cha mtoto wake kubainisha hivyo pia.

Rowan Leach mwenye umri wa miaka 20, ambaye alikuwa akimlea mtoto wake peke yake alibaini kifo cha mtoto wake mara baada ya kuamka saa sita usiku kumnyonyesha mtoto huyo na kumkuta hapumui.

Mama huyo aliwaelezea wapelelezi wa chanzo cha kifo cha mtoto wake wakati akisubiri huduma ya dharura ikamilike.

"Kifo cha mtoto wangu kimenisikitisha sana"Bi.Leach ambaye alimpoteza mtoto wake Hadley alieleza.

Licha ya kwamba mtoto huyo alikimbizwa hospitalini,wahudumu wa afya walishindwa kuokoa maisha ya mtoto huyo hivyo kufariki majira ya alfajiri mwezi septemba mwaka jana.

Bi.Leach kutoka Southampton alikuwa anamlea mtoto wake kwa usaidizi wa mama yake.

Alielezea hali ilivyokuwa kabla ya mtoto wake kufariki,mama huyo anasema alipitiwa na usingizi mara baada ya kumchukua mtoto wake na kumfunika kwa koti lake kwa sababu kulikuwa na baridi kali na lengo lake lilikuwa ni kumnyonyesha baada ya muda.

"Nilishangaa kumkuta mtoto wangu yuko upande wa pili wakati alikuwa amelala upande mwingin," Bi.Leach alieleza.

Mchunguzi mkuu Grahame Short ambaye hakuweza kuelewa kwa haraka chanzo cha kifo cha mtoto huyo kilitokeaje lakini alisema hamlaumu mama huyo kuwa mzembe.

Aliongeza kwa kudai kwamba huwa anawaonea huruma akina mama ambao wanahudumia watoto peke yao bila ya kuwa na wenza wao.

Vilevile uchunguzi uliofanywa haujaleta hali yeyote iliyotiliwa mashaka maelezo ya mama huyo ya namna mtoto wake alivyokufa.

Takwimu zinaonesha kwamba idadi wa watoto 133 wamefariki katika miaka mitano iliyopita kutokana na tabia ya akina mama wanaolala na watoto wao ,kwa mujibu wa data za elimu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kichwa cha habari tofauti na habari yenyewe...sijaona mahali waliposema sababu au ni kwanini tusilale na watoto usiku..

    ReplyDelete

Top Post Ad