Lissu aeleza atakachofanya kwa siku 100

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Tundu Antipas Lissu katika muendelezo wa kampeni zake jijini Dar es salaam ambapo leo Agosti 30 zimefanyika katika viwanja vya Liwiti Tabata amesema Nchi inahitaji maridhiano ya kitaifa. 


Amesema katika siku 100 za kwanza baada ya kupata ushindi katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 28, ataunda tume kwa ajili ya upatanishi na ukweli ili kuvumbua mabaya yanayofanyika katika nchi. 


‘‘Nikiingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu mwaka huu katika siku 100 za kwanza nitaunda Tume ya upatanishi na ukweli ili tufahamu mambo yote haya mabaya ambayo yamefanyika katika nchi yetu, tuwafahamu walioyatenda, tufahamu kwanini waliyatenda, nani aliyewatuma halafu tuwaambie tubuni dhambi zenu’’ amesema Lissu. 


Aidha Mgombea huyo amedai kuwa lengo sio kulipa kisasi bali wanataka kufahamu ukweli ambao utawaweka huru.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad