AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Moussa Dembele aliingia uwanjani akitokea kwenye benchi la wachezaji wa akiba na kufunga mabao mawili ya dakika za mwisho wakati Lyon ikisababisha mshangao mwingine wa Ligi ya Mabingwa jana usiku, kwa kuiondoa Manchester City ya Pep Guardiola na ushindi wa mabao matatu kwa moja wa robo fainali mjini Lisbon.
City ilionekana kuwa kwenye mkondo sahihi wa kushinda mechi hiyo baada ya bao la Kevin De Bruyne katikati ya kipindi cha pili kulifuta bao la ufunguzi la Maxwel Cornet katika kipindi cha kwanza.
Lakini mambo yakaharibika wakati Dembele alipotumia makosa ya wachezaji wa City na kuipa Lyon ushindi. Lyon sasa itacheza nusu fainali Jumatano dhidi ya Bayern Munich.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK