Majadiliano na Urusi Kuhusu Chanjo ya Corona Yanaendelea – WHO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Shirika la Afya Duniani, WHO barani Ulaya limesema limeanza majadiliano na Urusi kujaribu kupata taarifa zaidi kuhusu chanjo ya ugonjwa wa COVID-19 ambayo imeidhinishwa na nchi hiyo hivi karibuni. Wiki iliyopita, Urusi ilikuwa nchi ya kwanza duniani kutoa ridhaa ya kutumika kwa chanjo ya virusi vya corona wakati Rais Vladmir Putin alipoiidhinisha chanjo hiyo.


Hata hivyo, chanjo hiyo bado haijafanyiwa majaribio yanayotakiwa ili iweze kuidhinishwa kutumika. Catherine Smallwood, afisa wa ngazi ya juu wa dharura wa WHO barani Ulaya amesema shirika hilo limeanza mazungumzo ya moja kwa moja na Urusi.

Smallwood amesema maafisa wa WHO wameanza kubadilishana taarifa kadhaa ambazo zinahitajika kufanyiwa tathmini na shirika hilo. Mkurugenzi wa WHO barani Ulaya, Dokta Hans Kluge amesema shirika hilo limefurahishwa na maendeleo ya chanjo hiyo, lakini kila chanjo lazima iwasilishwe kwenye hospitali zao kwa ajili ya majaribio.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad