Messi Atua Man City

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



VYOMBO vikubwa vya habari nchini Hispania vimeripoti kwamba baba mzazi wa Lionel Messi, mzee Jorge Messi, amewasili katika jiji la Manchester kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kufanya mazungumzo na Club ya Man City juu ya uhamisho wa mwanaye, Lionel Messi,  ambaye ameshaomba kuihama Barcelona.

Messi anaripotiwa kuvutiwa zaidi na Man City ili kuungana tena na kocha wake wa zamani, Pep Guardiola. Messi ameshatangaza kuwa yuko huru kuondoka Camp Nou, kitendo ambacho kimefanya mashabiki kuandamana kushinikiza  klabu hiyo isimruhusu kuondoka.

Manchester City anapewa alama 5/2 kumnunua staa huyo wa timu ya taifa ya Argentina.

Kwa mujibu wa Ripoti ya RAC1 na TyC Sports vimeeleza kuwa kuna mazungumzo ya Messi kujiunga na miamba hao wa soka kwa mkataba wa miaka miwili japo bado ni tetesi na hazijawekwa wazi na iwapo atalipwa uhamisho kwa sababu yeye ndiye ameomba kuondoka.






-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad