Mrisho Ngasa Awaaga Mashabiki wa Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



MRISHO Ngassa kiungo mshambuliaji wa Yanga leo amewaaga rasmi mashabiki wake kwa kusema kuwa msimu ujao hatakuwa ndani ya kikosi cha Yanga. 


Kupitia ukurasa wa Instagram,Ngassa ameandakika hivi:-"Kwanza nitoe shukrani zangu kwa wote tuliokuwa pamoja katika kipindi chote, Yanga viongozi wangu mashabiki na wachezaji wenzangu kwa kikao kilichofanywa leo sitakuwa katika kikosi cha Yanga niwatakie mafanikio yalio mema. Enjoy soccer. 


Yanga kwa sasa inafanya maboresho ya kuimarisha kikosi kwa ajili ya kuongeza nguvu kwa msimu wa 2020/21. 


Kwa msimu wa 2019/20 Ngassa alikuwa miongoni mwa wazawa ambao walikuwa wanatimiza majukumu yao na alitoa pasi ya mwisho kwenye ushindi wa bao 1-0 mbele ya Lipuli Uwanja wa Samora. 


Mchezo wake wa mwisho ilikuwa ni Julai 26 wakati wakisepa na pointi tatu zilizoipa nafasi Yanga kumaliza ikiwa nafasi ya pili na pointi 72.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad