Mwanamume aliyekuwa akisakwa sana na FBI Kwa Mauaji ya Wanawe akamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Yaser Abdel Said mwenye umri wa miaka 63 alikua anasakwa na FBI kuhusiana na mauaji ya wanawe wa kike kwa miaka 12


Dereva wa taxi ambaye amekuwa akitafutwa kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya binti zake wawili amekamatwa baada ya kwenda mafichoni kwa miaka 12 iliyopita.


Waranti ya kumkamata Yaser Abdel mwaka 2008 baada ya kuwapiga risasi binti zake, Sarah Yaser Said, 17, na Amina Yaser Said, 18.


Mshukiwa huyo mzaliwa wa Misri aliwekwa kwenye orodha ya shirika la upelelezi la Marekani FBI, ya watu 10 wanaotafutwa zaidi mwaka 2014.


Mtu huyo aliye na umri wa miaka 63- hivi karibuni atahamishwa Kaunti ya Dallas, ilisema taarifa iliyotolewa na Idara ya FBI Dallas siku ya Jumatano.


Jopo kazi la uhalifu wa ghasia linaloongozwa na FBI mjini Dallas limekuwa likimtafuta kwa muda mrefu Yaser Abdel," alisema ajenti maalum wa FBI Dallas, Matthew DeSarno.


"Wachunguzi hawa wenye tajiriba hawajawahi kuchoka kumtafuta kwani waliahidi kuwapa haki wahasiriwa katika kesi hii."


Mama ya wasichana hao, Patricia Owens, amesema amefurahishwa na hatua ya kukamatwa kwake, na kuambia vyombo vya habari vya mji huo: "Sasa wasichana wanaweza kupumuzika kwa amani ."


Islam Said, mwana wa kiume wa mshukiwa, na Yassim Said, ndugu yake mshukiwa walishitakiwa kwa, kumficha mtoro huyo.


Uchunguzi wa mauaji ulianzishwa Januari mosi 2008 baada ya Amina na Sarah kupatikana wakiwa wameuawa kwa kupigwa risasi.


Siku hiyo, mshukiwa aliwabeba kwenye taxi wasichana hao kwa kisingizio kwamba anaenda kuwanunulia chakula, FBI inadai.


FBI inasema aliwapeleka hadi Irving, Texas, ambako inadaiwa aliwapiga risasi wasichana hao ndani ya gari. Wote walifariki kutokana na majeraha kadhaa ya risasi.


Kabla ya vifo vyao, jamaa wa familia aliwaambia polisi kwamba mshukiwa alitishia "kumdhuru" Sarah kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu ambaye sio Muislamu, kwa mujibu wa kituo cha habari cha CBC.


Mauaji ya mwanafamilia anayedhaniwa kufedhehesha jamaa zake wakati mwingine husemekana kuwa "mauaji ya heshima" - lakini wakosoaji wanapinga maana inayotolewa kwa mauaji kama hayo.


Idara ya polisi ya Irving ilifanya uchunguzi wa mauaji ya Amina na Sarah na, kufikia Januari 2, 2008 waranti ya kukamatwa kwa Yaser Abdel Said ilitolewa.


Tangu wakati huo, maajenti wa FBI "wamekuwa wakipambana kuwatafutia haki Amina na Sarah",Mkuu wa Idara ya polisi ya Irving Jeff Spivey, alisema.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mpenzi wangu aliachana na mimi, najua ilikuwa kosa langu ambalo lilimfanya aachane na mimi, akanipata nikiongea juu yake, kuna kijana niliyemwita rafiki yangu alinivuta na kufanya naye mapenzi kisha mpenzi wangu akatushika, basi aliachana na mimi, ninampenda sana, nilifurahisha kwa wiki na miezi hakukubali kunikubali, nilikuwa nikisoma mkondoni jinsi ya kumrudisha mpenzi wangu basi nilikuta na makala juu ya jinsi mwanamke alirudi Mumewe aliyempa talaka, alisema kuwa Dk Lomi amsaidia alifanya sala kadhaa na mumewe amerejea kwake, basi na mimi nikawasiliana na Dr Lomi na kuelezea kile kilichotokea kisha akanisaidia kufanya maombi kadhaa na mpenzi wangu akarudi akiniombea alijuta kuwa bado ananipenda na leo tumerudi pamoja na naahidi kamwe hatutazungumza juu yake na leo tunafurahi, ikiwa unahitaji pia Msaidizi wa Dk Lomi kuwasiliana naye kwenye Line ya nambari ya WhatsApp; +2349034287285 unaweza pia kumtumia barua pepe; lomiultimatetemple@gmail.com kwa msaada

    ReplyDelete

Top Post Ad