Mwanaume wa Miaka 69 Anataka Kupunguza Miaka 20 ya Umri wake Kisheria

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkufuzi mahiri kutoka Uholanzi anataka kubadilisha umri wake kisheria na kuongeza matarajio yake ya mahusiano ya kimapenzi.

Emile Ratelband mwenye umri wa miaka 69, anataka kubadilisha siku yake ya kuzaliwa kutoka mwezi Machi 1949 mpaka kuwa Machi 1969, akilinganisha na mabadiliko ya kubadilisha jinsia.

"Tunaishi katika wakati ambao unaweza kubadili jina lako na kubadili jinsia yako.

Kwa nini siwezi kuwa na maamuzi ya umri wangu?" Ratelband alisema.


Kwanini hekalu la shetani linawashtaki watayarishaji wa kipindi cha Sabrina
Mahakama moja mashariki mwa mji wa Arnhem inatarajia kusikiliza kesi hiyo nadini ya wiki nne zijazo.

Hata hivyo mamlaka ilitilia shaka kesi hiyo wakiamini kuwa hakuna sheria ambayo inamruhusu mtu kubadili siku yake ya kuzaliwa ,Vyombo vya habari vya nchi hiyo viliripoti.

Jaji mmoja ametaka kujua ni nini ambacho kitatokea baada ya bwana Ratelband kutaka kupunguza miaka yake 20.

"Wazazi ambao watakuwa wanakuangalia watakuwa ni kina nani?Huyo mtoto mdogo alikuwa nani?" Jaji aliuliza.


Ratelband amedai kuwa huwa anahisi kutengwa kwa sababu ya umri wake.

Na hali hiyo huwa inamkosesha fursa za kupata ajira na kufanikiwa kupata wenza katika tovuti ya Tinder.

"Nikiwa nna umri wa miaka 69, ni kama nimefungwa. Kama nikiwa na miaka 49 basi nnaweza kununua nyumba mpya na magari ya aina tofauti tofauti.


Aliongeza kwa kudai kuwa akiwa kwenye mtandao wa Tinder ambao unasema umri wake ni 69,huwa hapati majibu.

Hivyo akiwa na umri wa miaka 49 na kwa muonekano wake ulivyo basi anaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kifahari.

Ratelband amesema kwamba kwa mujibu wa daktari wake, mwili wake ni wa mtu mwenye umri wa miaka 45 na kujielezea mwenyewe kuwa yeye ni mungu mdogo.

Aliandika kwenye ukurasa wa Facebook mwaka jana na kuelezea namna ambavyo aliamua kuchukua uamuzi huo.

Sasa nina uume mpya nina matumaini ya kupata mpenzi
Alidai kwamba alifanya uamuzi huo siku moja alipokuwa anajiangalia katika kioo na sio kwa sababu alikuwa na hofu ya kuwa mzee lakini anataka kuishi muda mrefu awezavyo.


Ratelband anafanya kazi katika vyombo vya habari na mhamasishaji ambaye pia ni mkufuzi wa vipindi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad