Mwandishi wa habari wa Kenya aachiliwa Ethiopia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kitendo cha kukamatwa kwa Yassin Juma kililaaniwa dunianiImage caption: Kitendo cha kukamatwa kwa Yassin Juma kililaaniwa duniani


Mwandishi wabari wa Kenya Yassin Juma ameachiliwa huru kutoka mahabusu nchini Ethiopia – takriban wiki moja baada ya wakili wake kusema kuwa alipatwa na maambukizi ya virusi vya corona gerezani.

Amehamishiwa kwenye hospitali ya serikali kwa ajili ya matibabu, na ataruhusiwa kusafiri kurejea nyumbani Kenya baada ya kupona.

Bwana Juma,ambaye ni mwandishi huru wa habari, alikamatwa katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa, mwezi wa Julai, kufuatia ghasia zilizoibuka baada ya kuuawa kwa mwanamuziki maarufu wa jamii ya Oromo Hachalu Hundessa 

Maafisa nchini Ethiopia wiki hii waliamuru kuachiliwa kwake, wakisema “alikamatwa kimakosa”.

Wizara ya Mambo ya nje ya Kenya ilisema kuwa aliachiliwa baada ya ubalozi wake nchini Ethiopia kuingilia kati na ambao ulipinga kushikiliwa kwake.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad