Ofisi za CHADEMA zachomwa, waeleza kilichojiri

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa CHADEMA Tumaini Makene amesema kuwa tukio la ofisi za chama hicho Kanda ya Kaskazini kuchomwa moto na wasiojulikana si jambo jema ukizingatia leo Mgombea Urais wa chama hicho Tundu Lissu atakuwa Arusha.


Makene ametoa kauli hiyo hii leo Agosti 14, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, na kuongeza kuwa na hata mlinzi wa ofisi hizo mpaka sasa hivi hajulikani alipo na hata simu zake hazipatikani.

"Taarifa za awali usiku wa kuamkia leo watu wasiojulikana wamevamia na kumwagia Petroli jengo la Ofisi za Kanda ya Kaskazini,  na bahati mbaya hata mlinzi wa ofisi hizo hajulikani yuko wapi baada ya tukio hilo, ni tukio baya kwa sababu hata mgombea wetu wa Urais anaingia Jiji la Arusha leo" amesema Makene.

Ofisi za chama hicho Kanda ya Kaskazini zimeungua moto usiku wa kuamkia leo, baada ya watu wasiojulikana kumwagia Petroli jengo hilo na kisha kulilipua.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. What a Dramatic Scene..!!!

    The only one to expllain its planning and execution is not other than Godiless Faru Joni and Mlinzi.
    ukizingatia kuanzia J4 baadhi ya vitu vilianza kutolewa kwa ajili ya maatayarisho ya tukio for Media propaganda. Mmekula kwenu.

    ReplyDelete
  2. What a perfect Dramatic Scene..!!!

    The only one to explain, its planning stage and its execution is non other than Godiless Faru Joni and Mlinzi.
    ukizingatia kuanzia J4 baadhi ya vitu vilianza kutolewa kwa ajili ya maatayarisho ya tukio for Media propaganda. Imekula kwenu.

    ReplyDelete

Top Post Ad