Onyango wa Simba ashangazwa na wanaomuita mzee

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Beki mpya wa Klabu ya Simba, Joash Onyango ameshangazwa na mashabiki na wapenzi wa kandanda wanaomuita mzee wakati yeye bado kijana.

Onyango ambaye alijiunga na Simba wiki chache zilizopita akitokea Gor Mahia ya Kenya, amesema inawezekana watu wanamuita mzee kutokana na kupaka rangi nyeupe nywele na ndevu zake.

''Nafikiri wengi wananiita mzee kutokana na rangi niliyopaka kwenye nyele na ndevu zangu,lakini kwa kweli sina haja ya kufikiria wao wanachosema''

EATV ilipomuuliza kuhusu umri wake alisema''Umri ambao mnasikia unatajwa na watu utakua ndio huo huo'' alisema Onyango.

Kuhusu kuja Simba, Onyango amesema ilikua ni ndoto yake kuja kucheza na rafiki zake aliocheza nao nchini Kenya kama Meddie Kagere na Francis Kahata ambao wote walikua Gor Mahia.

Katika hatua nyingine, Onyango alisema atahitaji kuonyesha umahiri wake ili apate namba kwa kuwa Simba ina wachezaji wazuri katia idara anayoichezea ambayo ni ya ulinzi
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad