PIcha ya Mtu na Mama yake Wakiwa Naendesha Ndege Kubwa Kabisa ya Delta Airlines Yazidi Kuzua Gumzo Duniani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kuna siku kwenye ndege ya shirika la Delta airlines iliyokuwa ikitoka Los Angeles kwenda Atlanta kuna binti mmoja mdogo akamuomba muhudumu wa ndege aende akaangalie chumba cha marubani kilivyo. Wahudumu walimruhusu na wakampeleka.

Baada ya muda alitoka akiwa so excited mpaka anashindwa kuongea.  Kuna jamaa akajikuta anatamani kujua mtoto kashangazwa na nini,  naye akaomba kwenda. Awali Wahudumu walimkatalia lakini Ali insist mpaka wakamruhusu.

Huyo jamaa anaitwa Dr. John. R. Watret ambaye ndiye aliyepiga picha hii walipotua na kuituma tweeter, akaandika "Nilikuwa kwenye ndege kutokea Los Angeles kwenda Atlanta,  cha kushangaza kwenye chumba cha marubani kulikuwa na wanawake wawili ndio walikuwa wakiendesha ndege hiyo. Lakini cha kushangaza zaidi marubani wa kike hao ni mama na binti yake wa kumzaa ".

Yes hao ni mama Captain Wendy Rexon na binti yake First officer Kelly Rexon waajiriwa wa shirika la ndege la Delta airlines wakiwa na uwezo wa kurusha ndege zote kubwa za shirika hilo ingawa mama anasema ni nadra sana kupangwa pamoja Kama ilivyotokea kwenye flight hiyo. Ni tukio nadra Sana kutokea duniani kiasi Kwamba tweet ya Dr John ilikuwa shared duniani na watu 16,000 ndani ya muda mfupi sana.

Baada ya tweet hiyo vyombo vya habari mbalimbali vilianza kuwatafuta kwa ajili ya kuwahoji na walishangazwa zaidi mama alipowaambia kuwa ana binti yake mwingine aitwaye Kate Rexon ni rubani pia. Lakini baba yao Kate na Kelly ni rubani mstaafu pia.

*Anyway kwa kifupi: Wanawake mnaweza komaeni tu
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad