RPC Morogoro aeleza ajali ya costa ya abiria kubanwa na kontena na kujeruhi watu 4

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa jumla ya watu 10 wamejeruhiwa huku 4 kati yao wakijeruhiwa vibaya, baada ya gari waliyokuwa wakisafiria kukandamizwa na Kontena ambalo lilikuwa limebeba Tumbaku katika eneo la Nanenane mkoani humo hii leo.



Ajali ya Lori na Costa, mkoani Morogoro.


Kamanda Mutafungwa amesema kuwa ajali hiyo imetokea hii leo Agosti 17, 2020 majira ya saa 3:00 asubuhi, ambapo gari aina ya Costa ilikuwa ikitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Morogoro na ndipo ilipolivagaa Lori hilo ambalo lilikuwa limepata hitilafu iliyopelekea Tela lake kukatika na hivyo kuziba njia yote.


“Tela hilo lilikatika hivyo kusababisha Tela lililokuwa limebeba tumbaku kukata barabara yote na ndipo gari aina ya Costa iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam iliweza kuingia ubavuni kabisa mwa hilo Tela, tumeokoa jumla ya watu 6 wamepelekwa Hospitali na hali zao ni nzuri, lakini pia tumetoa watu 4 ambao walikuwa mbele kabisa na walikuwa wamekandamizwa na hali zao ni mbaya” amesema Kamanda Mutafungwa.


Aidha Kamanda Mutafungwa amesema kuwa majeruhi wote wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya matibabu.



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad