Wanawake waandamana katika mji mkuu wa Belarus kumtaka rais Lukashenko kujiuzulu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Maelfu ya wanawake waliandamana katika mji mkuu wa Belarus, Minsk hapo jana wakipeperusha bendera, maua na maputo katika mfululizo wa maandamano ya hivi punde dhidi ya serikali ambayo yameikumba nchi hiyo tangu kufanyika kwa uchaguzi wa urais uliokumbwa na utata mwezi huu. 


Wanawake hao waliandaa maandamano hayo waliyoyaita maandamano ya umoja na kutoa wito kwa Lukashenko na serikali yake kujiuzulu. 


Rais Alexander Lukashenko amekanusha madai ya upinzani kwamba aliiba uchaguzi huo wa Agosti 9 kurefusha uongozi wake wa miaka 26. 


Barabara ambazo zilitumika katika maandamano hayo zilifungwa na polisi na vikosi vya ulinzi. 


Maandamano madogo kama hayo yalifanyika katika miji mingine. 


Lukashenko amesema kuwa waandamanaji hao wanafadhiliwa na mataifa ya Magharibi na kuishtumu jumuiya ya kujihami ya NATO kwa kuongeza vikosi katika mipaka yake madai yaliyokanushwa na jumuiya hiyo. 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad