WATU Wengi Hawamuelewi NYOKA Ndio Maana Wanapanic, Chukua Tahadhari Hizi Pindi Uking'atwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


WATU Wengi Hawamuelewi NYOKA Ndio Maana Wanapanic, Chukua Tahadhari Hizi Pindi Uking'atwa
Wengi wakimuona nyoka wanaanza kukimbia ,kupiga makelele.Nani kakuambia kuna nyoka ambaye akimuona mtu anaanza kumkimbiza.

Nyoka sio simba au chui ambao tabia zao wakimuona mtu ambaye ni kitoweo kwao wanaanza kumkimbiza kwa nia ya kumla.Kwa nyoka la hasha hakuna nyoka wa aina hiyo awe venomous au non venoumous.Nyoka huwakimbiza rodents tu kama panya sababu ni kitoweo chao.



Watu hawamtizami nyoka kama kiumbe wa porini Bali humtizama kama vile kitu kibaya hilo ndio tatizo.

Nyoka pekee ni kiumbe namba moja ambaye watu humuelewa sivyo ndivyo Africa,hivyo ni mnyama anayeongoza kuuliwa kikatili

Nyoka hupata attention mbaya sababu ya stori ambazo watu husikia pale mtu anapong'atwa

Kung'atwa kwingi panatokea pale mtu anapojaribu kumzuru nyoka na kiumbe huyo anajaribu kujitetea

Majira ya kiangazi nyoka hujificha sana chini ya mawe,miamba majani au kwenye miti kukaa mbali na joto la jua

Mida ya jioni hujitokeza kwa wingi na usiku wakati hali ya joto ipo chini hushamili kwa wingi

Nyoka wadogo sumu yao sio hatarishi sana kama nyoka wakubwa.Mfano Brown snake kila akiwa mzee sumu yake ndio inakuwa kali zaidi


Njia nzuri ya kufanya pindi ukimuona nyoka mwache pekee yake usimbughudhi labda kama atahatarisha maisha ya watoto

Utajiingiza kwenye matatizo pindi ukimsogelea na kuanza kumrushia fimbo ,nyoka ataamua kujilinda na kujilinda kwao ni kutafuta timing ya kukugonga ila kabla ya kufanya hivyo atakupa alarm ya kufungua mdomo wake na kurudi nyuma.

Endapo mtu aking'atwa na nyoka yafuatayo ni yakufanya.

1.Mtulize mgonjwa awe katika hali ya utulivu,asipanic sababu akipanic atasababisha moyo uende mbio hivyo msukumo wa damu utakuwa wa kasi na hivyo kurahisha usambaaji wa sumu kwenda kwenye moyo

2.Kama nyoka yupo sehemu husika usimuue au kumkamata

3.ondoa vitu vyote kwenye mwili wa mgonjwa ambazo zinazuia mzunguko wa damu kama saa,mkanda ,Pete, viatu sababu vitaweza kumletea matatizo

4.safisha eneo lililong'atwa ila usichue au kusugua sababu itaweza kusababisha sumu iliyo nje iweze kuingia.

5.Mzuie ngonjwa asitembee hovyo na mbebe mgonjwa sababu ukimuacha atembee sumu itasambaa kwa kasi sana

6.Funga bandage na weka pressure kwa juu


7.Mchukue mgonjwa na mpeleke kwenye hospitali ya karibu haraka iwezekanavyo lakini kwa kipando


Usimpe chakula chochote au maji mgonjwa haswa pombe

Usiweke barafu kwenye sehemu iliyong'atwa

Usikate sehemu iliyong'atwa na kufyonza hakuna uthibitisho wa kisayansi unaosema hivyo pia hiyo njia inaweza kumletea madhara anayefonza

Usimpe pain killers mgonjwa au dawa yeyote ilei


Mwisho itolewe elimu kwa wachungaji na wakulima na haswa watoto wanaotumwa kuchunga mifugo

Kuna stori ya kusikitisha ilitokea Zimbabwe miaka 3 iliyopita kijana mmoja wa umri wa miaka 13 alikuwa anasoma darasa la 7 moja ya masiku alikuwa anachunga mifugo pamoja na wadogo zake 2 ,katika hali ya taharuki Nyoka aina ya black mamba alimgonga kijana yule mkononi sababu kijana yule alikatiza kwenye mti ambao black mamba alikuwa amejituliza baada ya kung'atwa wadogo zake walimuambia waende nyumbani wakawaeleze wakubwa wao kilichotokea lakini kijana yule alikataa alisema ni nyoka wa kawaida na hali ni ya kawaida akachukua kitambaa na kujifunga na wakaendelea kuchunga.Haikupita muda mrefu 30mins kijana yule akawa anasikia kizunguzungu na kudai haoni na anasikia ugumu kupumua na inavyoelezwa ngozi ya kijana yule ikawa inabadilika rangi na kuwa nyeusi wale wadogo Zake wakambeba kumrudisha nyumbani lakini ikawa too late .kifo cha mtoto yule kilivuta hisia ya watu wengi

Hivyo elimu kubwa itolewe kwa wakazi wa vijijini ,wakulima ,wafugaji njia ya kutumia mawe asilimia ,kukata na kuanza kufyonza sio sahihi.

By undefine
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad