Afariki DUNIA Akidungwa Sindano ya Kuongeza Makalio

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Daktari mmoja nchini Marekani, Donna Francis ameshtakiwa mara baada ya kusababisha kifo cha mwanamke wa miaka 34 aliyekuwa anamfanyia upasuaji wa kuongeza makalio.

Donna Francis amekiri mashtaka ya mauaji hayo yametokana na uzembe hali iliyopelekea daktari huyo kufungiwa leseni yake ya kufanya shughuli za kitabibu.

Alifanya upasuaji huo wa kuongeza maumbile kwa mwanamke huyo mnamo Mei, 2015, ambapo wakati wa upasuaji mgonjwa alipatwa na mshtuko wa moyo uliopelekea kupoteza uhai wake.

Inaelezwa kuwa kifo cha mwanamke huyo kilisababishwa na dawa ya kuongeza maumbile ambayo alichomwa sindano na daktari wakati wa matibabu.

Video: Kwa nini wanaume wagumu kuoa, Je tunahitaji upepo wa Kisulisuli? sababu zatajwa
Upasuaji huo ulimgharimu dola 16000 sawa na milioni 2 na zaidi kwa pesa ya kitanzania kwa ajili ya kuchomwa sindano hiyo ambayo ingemsaidia kuongea makalio, lakini bahati mbaya mara baada ya kudungwa sindano hiyo alipata mshtuko wa moyo na kupoteza maisha.

Fahamu sababu za kuzeeka kabla ya umri
Aidha, imekuwa utamaduni wanawake wengi karibu duniani kote kufanya upasuaji wa kuongeza au kupunguza baadhi ya sehemu zao za mwili hasa sehemu za makalio, matiti na kadhalika.

Japo yapo madhara mengi yanayotokana na mtindo huu wa maisha ambapo madhara hayo yanaweza kuwa ya muda mrefu au muda mfupi.

Tanzania wapo wadada ambao wamesafiri nje ya nchi na kutumia gharama nyingi sana kubadilisha mionekano yao kwa kuiongeza au kuipunguza kwa lengo la kuongeza mvuto zaidi.

Japokuwa teknolojia inakuwa na huu utamaduni wa kuongeza makalio unaweza ukaenda ukifa mara baada ya kugundua nguo za ndani ambazo tayari zimewekwa makalio bandia na hatua hii ni kufuatia madhara makubwa yatokanayo na kuongeza vitu bandia mwilini.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad