Akon Kuendelea na Ujenzi wa 'Akon City' Senegal

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii Akon wa muziki wa R&B nchini Marekani na ambaye amekuwa akizungumzia kujenga mji mpya nchini Senegal tangu 2018 amesema shughuli ya ujenzi itaanza mwaka ujao.

Akon hakuwatambulisha wawekezaji katika mradi huo lakini amefichua kwamba ufadhili wa thuluthi tatu ya dola bilioni sita imepatikana.

Mchoraji ramani wa mji huo mpya, Hussein Bakri, amesema idadi ya watu katika mji huo inakadiriwa kufika 300,000.

Akon, ambaye jina lake halisi ni Alioune Badara Thiam, aliwashirikisha moja kwa moja Wamarekani weusi katika mauzo ya mradi huo.

Alisema kuwa ametangamana na "Waafrika wenye asili ya Marekani ambao hawaelewi utamaduni wao, Kwa hivyo nilitaka kujenga mji ama kubuni mradi kama huu ambao utawapa motisha ya kuwa na makazi katika nchi yao," Shirika la habari la AFP lilimnukuu msanii huyo aliyezaliwa Marekani kutokana na wazazi raia wa Senegal, akisema.

"Unapoamua kuishi Marekani,Ulaya ama mahali kwengine ughaibuni na ungelipendelea kuzuru Afrika, tunataka Senegal iwe kituo chako cha kwanza," alisema.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad