Baada ya Muda Gani Unaruhusiwa Kufanya Mapenzi na Mkeo Baada ya Kujifungua?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Zoezi la kujifungua linafariji na kuchosha pia, ni la faraja sana kwa kuwa linakufanya uwe mama? Wiki 4 za mwanzo kwa mzazi zinaweza kuwa katika kumbukumbu zako kwa muda mrefu kwakuwa ni wiki za ‘majimaji’ tu – jasho, kunyonyesha na haja ndogo kutoa majimaji yote ya ziada mwilini mwako. Inashangaza hata kama mtu utakuwa na hamu ya kufanya mapenzi katika kipindi hicho.

Madaktari wanasema kuwa mwili wa mwanamke unahitaji wiki 6 kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Katika kipindi hiki cha wiki 6, mfupa wa nyonga na uti wa mgongo hurudi kwenye hali yake ya awali. Homoni zako pia zinajirekebisha sambamba na misuli iliyopo kwenye sakafu ya nyonga kupumzika wakati ikirudi kwenye hali yake iliyokuwa nayo mwanzo kabla ya kazi kubwa iliyotoka kuifanya ya kumbeba mtoto na kusaidia kwenye kumtoa wakati wa kujifungua.

Kwahiyo, mpaka kitakapofika kipindi hiki cha wiki 6, unashauriwa kutofanya mapenzi, lakini haimaanishi kwamba huwezi kufanya mambo mengine kama kumbusu, kumshikashika, au kumnyonya mwanaume wako, na yeye kukufanyia hivyo hivyo. Wanawake wengine wanasema kuwa chuchu zao huwa na hisia sana kutokana na kunyonyesha kiasi kwamba wanaweza kufika kileleni kwa kushikwa chuchu tu.

Lakini kuhusu dawa za kuzuia kubeba mimba katika kipindi hiki, mnashauriwa muwe na tahadhari kuhusu kutumia njia yoyote itayoathiri mfumo wa homoni. Hii ni kwa sababu itaathiri sana kiwango na ubora wa maziwa na itamsababishia mtoto kutopata lishe inayotakiwa. Pia, vidonge vyenye oestrogen vimethibitishwa kusababisha kupungua kwa kiwango cha maziwa kwa mama anayenyonyesha, na mara nyingine hupunguza ghafla sana.

Shirika la Afya Duniani linasisitiza mtoto anywe maziwa tu kwa muda usiopungua miezi 6 kisha uendelee kumnyonyesha mpaka atakapofikisha miaka miwili. Wazazi wengi wanaona hii inawatesa na wengi wao wanasema kwamba miezi 6 ya mwanzo ni muhimu sana.

Unashauriwa uzungumze na daktari wako kuhusu muda gani unaweza kurudia kufanya mapenzi na njia za kutumia kujikinga na mimba ya haraka na pia umuulize hasa kuhusu kutumia dawa zenye progesterone na madhara yake kwako. Vidonge hivi vinaathiri maziwa (kwa wingi na ubora) kwa kiwango kidogo zaidi ukilinganisha na vidonge vyenye oestrogen.

Mwili wako umefanya kazi kubwa sana ya kuleta kiumbe duniani. Sio tu kwa sababu ni utambulisho wako na kukufanya uitwe ‘mama’ na chochote utachofanya kitakachokufurahisha, utashangaa jinsi ulivyo na sehemu nyingi zinazoweza kukufanya upate raha.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad