Baharia wa meli ya kubeba ndege ya Marekani atoweka Ghuba ya Arabuni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Jeshi la wanamaji la Marekani limeendesha zoezi la kumtafuta baharia aliyetoweka kutoka kwenye meli ya USS Nimitz wakati meli hiyo ilipokuwa kwenye shughuli ya doria katika eneo la kaskazini la bahari la ghuba ya Arabuni. Tukio hili limezuka wakati ikiwepo mivutano na Iran. 

Zoezi hilo limeendelea usiku kucha hadi leo Jumatatu. Msemaji wa jeshi la wanamaji la Marekani lililoko Bahrain, kamanda Rebecca Rebarich, amesema mabaharia waliokuwa ndani ya meli hiyo ya kubeba ndege walitoa tahadhari ya kutoweka kwa bahari huyo jana magharibi baada ya kumtafuta na kumkosa baharia huyo. 


Hata hivyo kamanda huyo amekataa kutaja jina la baharia huyo aliyetoweka akitoa sababu ya kutoruhusiwa katika sheria ya jeshi hilo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad