Hivi Ndivyo Ulivyokuwa Mdahalo wa Kwanza Kuelekea Uchaguzi Marekani...Myukano Mkali Hasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Ilitabiriwa kuwa lengo la Donald Trump wakati wa mjadala huu lilikuwa kumkera Joe Biden - na ndani ya dakika chache kuanza kwake, ikawa wazi alipanga kufanya hivyo kwa kumkatiza mara kwa mara makamu wa rais wa zamani.

Hiyo imefanywa kwa msururu wa kurushiana maneno , ambayo ni pamoja na Trump kuhoji ujasusi wa Biden na Biden akimwita Trump kichekesho, akimnyamazisha, kwa hasira, "Je! Utanyamaza, jamani?"


Mara kwa mara, Trump akimrushia vijembe Biden, akiacha mwana Democrat huyo akicheka na kutikisa kichwa.

Mwendesha mdahalo Chris Wallace alitangaza kwamba virusi vya corona ilikuwa mada inayofuata na kwamba wagombea wote watakuwa na dakika mbili na nusu bila kukatizwa kujibu, Biden alidakia "Kila la heri kwa hilo''

Uh, ndio. Kusimamia hili inaweza kuwa kazi mbaya zaidi Marekani hivi sasa.

Akizungumzia virusi vya corona, hii kila wakati ilikuwa ngumu ngumu kwa rais - na ilikuja mapema katika mdahalo .. Alilazimika kutetea jibu ambalo limesababisha vifo vya Wamarekani zaidi ya 200,000. Alifanya hivyo kwa kusema hatua ambazo amechukua kuzuia vifo zaidi kutokea na kupendekeza Biden angefanya mambo kuwa mabaya zaidi.

Jibu la Biden lilikuwa kuzungumza kwenye kamera akiuliza watazamaji kama wataweza kumuamini Trump (kura zinaonesha kuwa sehemu kubwa ya Wamarekani hawakubaliani na namna Trump anavyoshughulikia janga hilo.

Trump alijisifu kuhusu ukubwa mikutano yake ya kampeni, iliyofanyika nje kwa sababu ndivyo "wataalam" - wakisisitiza neno hilo - wanavyoeleza. Kisha akasema Biden alifanya mikutano midogo kwa sababu hakuweza kuvutia umati mkubwa.

Inawakilisha tofauti ya kimsingi katika njia ambayo wagombea wawili wanavyolitazama janga hilo na ikiwa hali inazidi kuwa nzuri - au mbaya zaidi.

Trump anagusia rekodi yake ya kufanikisha mambo

Ikiwa kuna ujumbe kampeni ya Trump inataka Wamarekani kuchukua kutoka kwa mjadala huu - kipande cha picha ya video ambacho kilitumwa kwenye akaunti ya rais hata wakati mdahalo ulikuwa ukiendelea - ni kwamba Joe Biden alikuwa na karibu nusu karne katika ofisi ya Umma kutatua shida zinazokabili nchi, na shida hizo bado zipo.

"Katika miezi 47, nimefanya zaidi ya vile umefanya kwa miaka 47," Trump alimwambia makamu wa rais.

Jibu la Biden lilikuja baadaye kwenye mdahalo.

"Chini ya rais huyu, tumekuwa dhaifu, wagonjwa, masikini na tumegawanyika zaidi," alisema.

Kuhusu hoja ya ushuru

Wakati habari ya New York Times kuhusu ushuru wa Trump ilipojitokeza Jumapili usiku, ilionekana kama bomu - umma ulikuwa ukiangalia taarifa ambayo rais alikuwa nayo, kwa kuvunja utamaduni, uliokuwa ukishikiliwa kwa miaka.

Wakati mada ilipokuja kwenye mjadala, Donald Trump alitoa utetezi kama huo kwa ule aliotoa mnamo 2016 - kwamba alikuwa amelipa ushuru mwingi na uwezo wake wa kukwepa muswada mkubwa wa ushuru ilikuwa tu kuchukua faida ya kisheria.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad