Hoja 9 za Ndugai Dhidi ya Tundu Lissu na Prof Jay

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


1. "Jimbo la Mikumi lilikuwa linaongozwa na mpinzani yeye na Wenzake kazi yao ilikuwa ni kupinga kila kitu, wao Kazi yao Kusema Siyo hadi bajeti yenye mshahara wake anapinga, Huyu wa Mikumi Kazi yake Bungeni ilikuwa akisimama ANASEMEA WANYAMA tu ila kuwasemea binadamu hapana"
Ndugai

2. "Ikulu haiachiwi ni mwiko, huwezi kuuza Mama Mkwe, tuliachiwa na Mwalimu Nyerere na Karume na chama chetu cha Mapinduzi hatuwezi waachia watu hawaeleweki"
Ndugai

3. "Hatuwezi waachia watu Ikulu wengine wamekuja jana wanatujaribu, katoka Ulaya jana anataka Urais haiwezekani lazima tumfundishe tarehe 28 Oktoba"
Ndugai

4."Nchi inaboresha usafiri wa Anga wanapinga, barabara wanapinga, Meli wanapinga hadi Vituo vya afya wanapinga ndo maana wakati mwingine kama Spika huwa nawatoa nje nawaambia haya tokeni nje mkapinge huko nje wanasema Ndugai Mkorofi"
Ndugai

5."Huyu Lissu nilimfukuza Bungeni kwa sababu ni mtoro alikua anazurura Ulaya anaisema vibaya nchi anasema nchi haina Uhuru amerudi hakuna aliyemkamata, anasema tunataka uhuru wakati Nyerere alishauleta anataka uhuru upi?"
Job Ndugai

6 "Hii ajenda ya uhuru na Haki sio yao ni ya Wazungu ambao wanataka Uhuru ule wa wasagaji na ushoga. Maana Hakuna Uhuru usio na Mipaka hata chama Chao Chenyewe hakina Uhuru. Hawana Ajenda ya Maendeleo hata moja wanayozungumza"
Job Ndugai

7. "Mgombea Tundu Lissu kila akipanda Jukwaani anasema Maneno machafu kwa Mama yake Rais Magufuli ni aibu kumtukana mama ni Laana, Mama yule anaumwa sio wa kutukanwa ni wa kuombewa"
Job Ndugai

8. "Rais wetu pia ana damu na nyama ni Binadamu, Huyu Lissu ni wa Ajabu Sana ni mchokozi anatafuta sababu ili aguswe namwambia kama kaka yake akome kumtukana mama yule sijui Lissu ni Binadamu au Mnyamapori"
Job Ndugai
Mjumbe

9. "Lissu haambiliki ni Mchochezi ni Jeuri ni kiburi sijui ana shida gani.Raha ya Tanzania kutaniana kufrahi na kucheka hii ndo Tanzania tunayoitaka sio Tanzania ya matusi, lawama wala Makasiriko"
Job Ndugai
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad